Majambazi hao waliitumia bunduki hiyo kwa kuvamia duka la vinywaji lililokuwa jirani na kuiba kiasi kikubwa cha pesa japo hakikuweza kufahamika kwa wakati huo.
Mtandao huu ulifanya juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Polisi Kinondoni, Camillus Wambura ili kupata undani wa tukio hilo na kiasi cha fedha kilichoibiwa ila simu yake ya mkononi ilipokelewa na msaidizi wake aliyedai kuwa kamanda alikuwa katika kikao.
(HABARI/PICHA: MAYASA MARIWATA NA SHANI RAMADHANI/GPL

