https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    MUDA WOWOTE ‘MAJEMBE’ HAYA YATAONDOKA KWENYE TIMU ZAO KABLA YA DIRISHA KUFUNGWA

    Daa..! Aisee nimekumbuka busara za muasisi wa taifa hili sana. Mzee
    Mandela nae alikuwa na busara sana na haiba ya mazungumzo, ila tayari
    majina ya Mwalimu na Mandela nimesha ya andika kwenye kitabu changu
    cha watu waliojaliwa utu na kuheshimu demokrasia. Hivi soka nalo lina
    busara au Malofa? Teh teh teh teh.. bila shaka umejibu lina Malofa,
    kwa kuwa mimi sijui maana ya Malofa inayokusudiwa ngoja niwaachie nyie
    ili mimi niendelee kutafuta busara na haiba ya mazungumzo hasa katika
    ukurasa huu ambao unasomwa na wanasoka kutoka kila kona ya dunia.
    Usajili bado unaumiza vichwa vya timu kibao za Ulaya hasa kutokana na
    kuanza kwa ligi na kuona mapungufu kibao kwenye vikosi vyao. Kutokana
    na hali hii, usishangae kuona baadhi ya sajili zikakamilishwa muda
    wowote kuanzia sasa. Jambo hili limenifanya nijaribu kupitia pitia
    baadhi ya mitandao ya Ulaya na kugundua baadhi ya sajili ambazo
    usishangae kuziona zimekamilika muda wowote kabla ya dirisha kufungwa.
    Hapa chini ni baadhi ya watu wanaotajwa kusajiliwa muda wowote kuanzia
    sasa kabla ya dirisha kufungwa… Ungana nami hadi mwisho, karibu
    sana,
    MARIO BALOTELLI- LIVERPOOL KWENDA AC MILAN
    MILAN, ITALY - FEBRUARY 03:  Mario Balotelli of AC Milan celebrates after scoring his second goal from the penalty spot during the Serie A match between AC Milan and Udinese Calcio at San Siro Stadium on February 3, 2013 in Milan, Italy.  (Photo by Claudio Villa/Getty Images)
    Mario ameshindwa kabisa kupata nafasi Anfield. Kutokana na kushindwa
    kufunga, yeye kama Mshambuliaji hana muda mwingine zaidi ya kwenda
    kutafuta maisha nyumbani kwao Italia. Japokuwa alisajiliwa kwa £16
    kutoka Milan, ila kwa sasa amekwenda kwa mkopo AC Milan kwani
    kulikuwa na kipengele kilichokuwa kinamruhusu kwenye mkataba wake kufanya hivyo. Timu
    zingine kama Sampdoria, Lazio na Fiorentina zilitajwa pia kumchukua
    kwa mkopo Mshambuliaji huyu mwenye asili ya Ghana.
    JOHN STONES-EVERTON KWENDA CHELSEA
    Kutokana na Mourinho kumkosa kabisa beki wa kati, Stones lazima atue
    Chelsea kwa dau lolote. £34 Milion, £40 milioni au zaidi zinaweza
    kutumika kutokana na kiwango kibovu cha mabeki wa kati wa Chelsea.
    Everton wameonekana kugoma ila Stones ameshaanza kuwasumbua ili
    wamruhusu aondoke kwenda Darajani.
    VICTOR WANYAMA-SOUTHAMPTON KWENDA SPURS
    balo
    Mkenya huyu amekuwa kivutio sana pale White Hart Lane, ila bado ana
    miaka miwili ya kucheza Saint Marry. Saint wasipomuuza sasa, watakuja
    kumuachia kwa bei ndogo sana kama watamuuza badae. Nathaniel Clyne
    alienda Anfield kwa bei ya
    kawaida kutokana na mkataba wake kuwa ukingoni, nazani Saint
    hawatakuwa tayari kuona hayo yanatokea tena kwa Wanyama. Kuna habari
    za uhakika ambazo ni za chini chini kwamba muda wowote Wanyama
    atakwenda London kufanya vipimo vya afya.
    LUCAS-LIVERPOOL KWENDA BESIKTAS
    Lucas ni kiungo mzuri japokuwa ameshindwa kupata nafasi ya kudumu
    kwenye kikosi cha Brendan Rodgers. Kutokana na kuhitaji kuonekana,
    Lucas amekuwa akisubiri ofa ya Besiktas kwa miezi kadhaa sasa.
    Inawezekana akasajiliwa kwa mkopo kwenda kucheza ligi ya Uturuki
    ambayo imeonekana kupokea ‘Makapi’ kutoka Epl mara kwa mara.
    ALEX SONG-BARCELONA KWENDA WEST HAM
    Kiungo huyu matata mwenye miaka 27 hana nafasi tena Camp Nou hasa
    kutokana na usajili walioufanya Barcelona msimu huu. Japokuwa
    aliondoka Barca kwa mkopo ila West Ham wana kila sababu ya kumsainisha
    hasa kutokana na umuhimu wake kwenye
    kikosi cha West Ham. The Hammer wana muhitaji sana Song kwani amekuwa
    akii-onganisha timu na hata kufikia hatua ya kupewa kitambaa cha
    unahodha. Barcelona wana mawili sasa, kumuacha abaki kwa mkopo au
    kumuuza kabisa kama wanavyoitaji West Ham.
    EMMANUEL ADEBAYOR-SPURS KWENDA WEST HAM
    balo 1
    West Ham wamekuwa wakimuhitaji tangu msimu uliopita Mshambuliaji huyu.
    Kutokana na West Ham kuwa wapinzani wa Spurs kwenye mbio za kuwania
    kucheza Europe League, Spurs walikataa kumuachia Adebayor msimu
    uliopita. Stoke, Aston Villa, Qpr na Crystal Palace pia wametajwa sana
    kumchukua Adebayor ila West Ham ndo wana nafasi kubwa ya kumchukua kwa
    mkopo Adebayor. Mwenyekiti wa Spurs, Daniel Levy yupo tayari kusaidia
    £100, 000 kama mshahara wa wiki kwa timu yoyote itakayomchukua
    Adebayor
    KEVIN DE BRUYNE-WOLFSBURG KWENDA MANCHESTER CITY
    Huyu Bwana mdogo amekuwa akizungumzwa pengine kuliko mchezaji yeyote
    anayetarajiwa kusajiliwa kwa kipindi hiki kifupi kilichobaki.
    Wajerumani wanahitaji zaidi ya £57 Millioni ili kumuachia Kevin,
    kiungo mshambuliaji ambaye alionekana mpuuzi pale Darajani. Muda
    wowote kuanzia sasa usishangae usajili huu kukamilika kwa pesa yoyote.
    SAIDO BERAHINO- WEST BROM KWENDA SPURS
    Kiungo huyu amekuwa akihitajika sana kwenda White Hart Lane kwa kitita
    cha £25 Millioni. Bila shaka usajili huu utakamilika muda wowote hasa
    kutokana na Berahino kutoonekana kwenye mechi dhidi ya Chelsea.
    Kukosekana kwake kunahusishwa sana na uhamisho wake wa chini chini
    kwenda London. Spurs wamekuwa wakihitaji viungo wanaocheza kama
    Berahino.
    Salym Juma
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MUDA WOWOTE ‘MAJEMBE’ HAYA YATAONDOKA KWENYE TIMU ZAO KABLA YA DIRISHA KUFUNGWA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top