Hapa ilikuwa meza kuu, yuko Freeman Mbowe (CHADEMA), Edward Lowassa (CHADEMA) na Prof. Lipumba (CUF)
Ulimwengu wa Siasa Tanzania August 06 2015 umepokea headlines nyingine zenye uzito ambapo aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba ametangaza kujiuzulu nafasi ya Uenyekiti wa Chama hicho.
Kwenye kile alichokisema wakati anatangaza kujiuzulu, yako na maneno mengine haya hapa >>> ‘Ni kweli nilishiriki kumkaribisha Lowassa UKAWA lakini dhamira na nafsi yangu inanisuta… Tumekaribisha watu wa CCM ambao waliipinga Rasimu ya Katiba, najiuliza tutaweza kusimamia malengo ya UKAWA‘ >>>> Prof. Lipumba.
Sentensi nyingine amesema hivi >>> ‘Taarifa ya kung’atuka niliitoa August 01 2015, nilisubiri kukamilisha masuala ya UKAWA ndio nitoke… Ninaendelea kuwa Mwanachama wa CUF na nimelipia Kadi ya Uanachama mpaka 2020, sina mpango wa Kujiunga ACT‘-Prof. Lipumba.
Hapa nina pichaz nyingine Kumbukumbu ya July 28 2015 siku Edward Lowassaalivyokaribishwa rasmi CHADEMA na UKAWA.


0 comments:
Post a Comment