https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    Wananchi watakiwa kupuuza propaganda za kuibiwa kura.


    Jumuia za kimataifa, waangalizi wa uchaguzi, wazanzibar na watanzania kwa ujumla wametakiwa kupuuza ghiliba na propaganda za kuibwa kura zinazoenezwa na viongozi wa vyama vya upinzani kupitia ukawa kwa kuwa madai hayo yana ajenda ya siri ya kuvuruga uchaguzi na amani ya nchi inayopangwa na viongozi hao kwa maslahi yao.
    Katika siku ya pili ya kampeni za uchaguzi zinazofanywa kwa pamoja na Dr Ali Mohamed Shein mgombea urais wa Zanzibar na Dr John Pombe Magufuli mgombea urais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania katika visiwa vya Zanzibar makamu wa rais wa Tanzania Dr Mohamed Gharib Bilal anaitoa kauli hiyo katika viwanja vya mnazi mmoja.
     
    Akizungumza na umati wa wananchi wa Zanzibar waliohudhuria mkutano huo katika viwanja vya mnazi mmoja Dr John Pombe Magufuli kwa upande wake mbali na kusisitiza suala la kulinda amani na muungano wa Zanzibar na Tanganyika serikali yake itaendelea kuzitatua kero nne za muungano zilizosalia sambamba na kulinda maliasili na rasilimali za taifa zinazovunwa bila ya kufuata utaratibu.
     
    kwa upande wake mgombea urais wa Zanzibar Dr Ali MohamedSshein amewataka watanzania kutoyumbishwa katika kudumisha suala la usalama na amani kwa kuwa ndio ngao pekee ya maendeleo ya taifa.
     
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Wananchi watakiwa kupuuza propaganda za kuibiwa kura. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top