Timu
kutoka kote Afrika zimewasili nchini Equatorial Guinea wakati ambapo
mechi za taifa bingwa barani zitarajiwa kung'oa nanga hii leo ikiwa ni
miezi miwili tangu taifa hilo la afrika ya kati likubal
i kuandaa mechi
hizo.Morocco ndiyo iliokuwa iandae kombe hilo lakini badala yake ikaomba kuahirishwa kwake kutokana na hofu ya kusambaa kwa ugonjwa wa ebola.
Shirikisho la kandanda barani Afrika CAF hata hivyo lilikataa ombi hilo la Morocco
Mkuu wa CAF (Hicham El Amrani) anasema kuwa kila tahadhari imechukuliwa nchini Equatorial Guinea kuwalinda watu kutokana na ugonjwa wa ebola.
Mechi ya kwanza itakuwa kati ya wenyeji Equatorial Guinea na Congo

