https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    MTIKISIKO; MAN CITY, CHELSEA, SPURS, SWANSEA, SOUTHAMPTON ZATOLEWA KOMBE LA FA

    250246C900000578-2925099-Yeates_centre_on_his_knees_celebrates_scoring_the_winning_goal_a-a-13_1422144972050
    Umdhaniaye siye ndiye. Michuano ya Kombe la chama cha soka cha Uingereza, FA, hatua ya nne (4) imeacha mshituko mkubwa pale vilabu vilivyopewa nafasi vilipofungashwa vilago na wale ambao awali walioonekana kama ‘vibonde’ 
    Chelsea 2 Bradford City 4, kwa umakini mkubwa klabu ya Bradford ilifanikiwa kurejesha goli mbili za haraka kutoka kwa Gary Cahil na Mbrazil, Ramires upande wa Chelsea na hivyo kuwang’oa vinara hao wa ligi kuu katika michuano hiyo tena katika dimba lao la ‘darajani’  Stamford Bridge.
    City wanashiriki ligi daraja la kwanza na mpaka dakika ya 38, walishakuwa nyuma kwa mabao 2-0, lakini walipambana vilivyo na kufuzu kwa raundi ya 5 ya michuano hiyo na hivyo kuzima ndoto ya vikombe vinne upande wa Chelsea msimu huu.
    Chelsea reject Filipe Morais levelled the fourth-round tie with 15 minutes to go before Jon Stead, the scorer of City’s first, teed up Andy Halliday for the winner eight minutes from time.
    And substitute Mark Yeates tucked in a stoppage-time fourth to inflict the Blues’ first home loss this season and spark jubilant celebrations from Phil Parkinson’s visitors.
    Manchester City 0 Middlesbrough 2, goli toka kwa nyota wa chelsea aliye kwa mkopo Patrick Bamford pamoja na shuti la Kike yalitosha kuiwezesha klabu inayowania kupanda ligi kuu ya  Middlesbrough kuwashitua na kuwashangaza mabinghwa wa tetezi wa taji la ligi kuu pale yalipowatupa nje kunako michuano ya FA
     Nyota huyo toka uingereza alitumiia vyema udhaifu wa safu ya ulinzi kabla ya Kike kuingia na kufunga akitokea benchi katika dakika za majeruhi dimbani Etihad ambapo siyo rahisi kuondoka na alama tatu kwa vilabu vingi
    City walitawala mchezo huo kunako kipindi cha kwanza lakini hata hivyo mlinda lango wa zamani wa miamba ya hispania anyecheza Boro, Tomas Mejias alikuwa kikwazo. Na kama vile haitoshi mpira ulopigwa na Frank Lampard uliguswa na kugonga mwamba dakika ya 89 kabla Kike hajawaadhibu kwa goli la pili.
    Southampton 2 Crystal Palace 3, ni mchezo ambao ulishuhudia jumla ya mabao matano yakifungwa huku ikishuhudiwa vijana wa meneja wa zamani wa Newcastle Alan Pardew wakitoka nyuma na kuwafunga ‘Saints’walio katika ubora wao.
    Awali, Graziano Pelle aliifungia “saints’ dakika ya tisa bao ambalo halikudumu kwani lilisawazishwa na mfaransa aliyepata kukipiga Arsenal Marouane Chamakh mda mfupi baadaye. Kisha baada ya mlinzi Scott Dann kujifunga, Palace wakasawazisha tena ndani ya dakika tano kupitia kwake nyota mwingine wa Arsenal aliye kwa mkopo klabuni hapo Yaya Sanogo. Baadaye Chamakh akatikisa tena wavu kwa mara ya pili na kuivusha klabu hiyo kwa hatua inayofuata
    Blackburn Rovers 3 Swansea City 1, miamba mingine ya ligi kuu iliyong’olewa kunako FA ni swansea pale mchezaji ambae taarifa zinadai anawaniwa sana na vilabun vya ligi kuu Rudy Gestede alipofunga bao maridhawa kwa upande wa Blackburn na kuwawezesha kuwatoa Swansea waliomaliza pungufu katika pambano hilo kwa ushindi wa bao 3-1
    Awali, mchezaji Kyle Bartley alitolewa nje kwa kadi nyekundu kunako dakika ya saba tu lakini bado Gylfi Sigurdsson alifunga bao murua kunako dakika ya 21 na kuiwezesha swansea kuongoza kwa muda pambano hilo. Iliwachukua dakika mbili tu Rovers kusawazisha kupitia kwake Chris Taylor na kisha mchezaji aliyetokea benchi Gestede, aliyepata pia kuichezea  Cardiff city akawatanguliza wenyeji kwa bao la pili zikiwa zimebaki takribani dakika kumi na mbili (12) pambano limalizike. Bao la tatu lilifungwa naye Craig Conway kunako dakika ya  89 ya pambano hilo.

    Tottenham Hotspur 1 Leicester City 2; Pamoja na kufunga mapema kupitia mkwaju wa penalti kufuatia madhambi alofanyiwa mshambulizi, Roberto Soldado bado totenham ilitolewa katika pambano lingine la kushangaza la mchuano wa kombe la FA. Mkwaju huo uliwekwa kimiani naye Andros Townsend, lakini haukutosha kwani  mabao toka kwa Leonardo Ulloa na Jeffrey Schlupp yalitosha kuwazima kabisa wenyeji dimbani kwao, White Hart Lane.
    Awali hali ilionekana kuwa mbaya kwa Leicester kwani siyo tu walifungwa penati hiyo kunako dakika ya 19 lakini pia walishuhudia kunyimwa na penati iliyofuatia na adhabu ya kadi ya njano kwa usajili wao mpya Andrej Kramaric kwa madai ya kujirusha.
    Hata hivyo, zikiwa zimebaki dakika saba tu, Leonardo Ulloa alifunga bao murua kisha mlinda lango wa Spurs Vorm akaruhusu mpira wa Schlupp kuvuka msitari na kuwapa leicester nafasi ya kufuzu hatua inayofuata.
    Katika michzo mingine za raundi hiyo, Nyota mnaijeria Victor Anichebe alifunga mara 2 ndani ya dakika 10 na kuwasaidia West Brom Albion kuwafunga wapinzani wao wa jadi  Birmingham City 2-1, Sunderland ikatoka suluhu tasa na Fulham katika pambano ambalo Jack Rodwell alitolewa nje kufuatia kadi mbili za njano. Timu hizo zitalazimika kurudiana tena kumpata mshindi. Reading nayo ikaifunga Cardiff 2-1, Derby ikaifunga Chesterfield 2-0 Darren Bent akifunga. Ilihali Preston ikambulia 1-1 dhidi ya Sheffield United. Wakati pambano la usiku Bolton Wanderers iliikomalia Liverpool na kuambulia sare pia.
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MTIKISIKO; MAN CITY, CHELSEA, SPURS, SWANSEA, SOUTHAMPTON ZATOLEWA KOMBE LA FA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top