Na Boniface Wambura
Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) limeizuia timu ya Polisi Mara kutumia Uwanja wa
Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma kwa mechi zake za Ligi Daraja la
Kwanza (FDL)
kuanzia leo mpaka hapo itakapotangazwa vinginevyo.
Uamuzi huo umechukuliwa kutokana
na matukio ya vurugu na uvunjifu wa amani ambayo yamekuwa yakitokea
kwenye mechi za FDL zinazochezwa kwenye uwanja huo, ikiwemo ile ya
Jumamosi iliyopita dhidi ya Mwadui ya Shinyanga ambapo waamuzi
walipigwa.
Kamati zinazohusika zitakutakana
hivi karibuni kupitia matukio yote ya utovu wa nidhamu kwenye FDL, na
hatua kali zitachukuliwa kwa wahusika ikiwemo na viwanja ambavyo
vimekuwa na sifa ya vurugu.
Vyama vya mpira wa miguu vya mikoa vina wajibu wa kutoa ulinzi wa kutosha viwanjani wakati wa mechi.

