https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    Rais Kikwete awateua mawaziri 8 Tanzania

    Rais Jakaya Kikwete
    Rais Jakaya kikwete wa Tanzania ametangaza mabadiliko katika baraza lake la mawaziri.
    Rais amewateua mawaziri wanane wapya pamoja na manaibu watano.
    Tangazo hilo lilifanywa na katibu katika ikulu ya rais balozi Ombeni Sefue.

    Mabadiliko hayo yanajumuisha wadhfa wa waziri wa nishati na kawi wa Profesa Muhongo ambaye amejiuzulu mapema leo pamoja na wadhfa wa waziri wa ardhi ambao uliwachwa wazi baada ya kupigwa kalamu kwa Anna Tibaijuka.
    Mawaziri hao wawili wanahusishwa na kashfa ya ufisadi ambayo ilimshinikiza mwanasheria mkuu pia kujiuzulu.Nafasi ya Profesa Muhongo imechukuliwa na aliyekuwa naibu wa waziri wa ardhi, George Simbachawene
    Rais Kikwete amewaapisha mawaziri hao wapya hii leo katika tangazo lililorushwa hewani na runinga ya taifa moja kwa moja.
    Hii ndio orodha ya mawaziri walioteuliwa
    MAWAZIRI
    George Simachawene waziri wa nishati na madini
    Mary Nagu- waziri wa nchi [afisi ya rais] mahusiano na uratibu
    Christopher chiza -waziri uwezeshaji na uwekezaji
    Harisson Mwakyembe[waziri wa ushirikiano wa afrika mashariki]
    William Lukuvi -waziri wa ardhi nyumba na makaazi
    Steven Wasira -waziri wa kilimo chakula na ushirika
    Samwel Sita -waziri wa uchukuzi
    Jenista Muhagama -waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera uratibu na bunge
    MANAIBU WAZIRI
    Stephen Masele -naibu waziri afisi ya makamu wa rais muungano
    Angela Kariuki -naibu waziri wa ardhi nyumba na makaazi
    Ummi Mwalimu- naibu waziri wa katiba na sheria
    Anna Kilango naibu waziri wa elimu na mafunzo ya kiufundi
    Charles Mwijage-naibu waziri wa nishati na madini
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: Rais Kikwete awateua mawaziri 8 Tanzania Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top