Miaka haisimami, siku
hazigandi na mshale wa saa hauna subira. Ndio hivyo unavyoweza
kuyazungumzia maisha ya mwanadamu, hatuna budi kuwa makini kuendana na
kasi hii. Ni kama ambavyo hayati Nelson Mandela akiamka leo Kisha
kumkuta Juan Mata akiwa katika benchi la Manchester United hana uhakika
wa nafasi mbele ya Ashley Young, Valencia na Januzaj.
Utahitaji kipawa cha
khali ya juu kumuaminisha mtu aliyepofuka mwaka Jana kuwa Mata
anazunguka mechi nne bila kuingia uwanjani lakini ndivyo ilivyo mchezaji
ambaye alikuwa kipaji mpaka kufikia kuitwa Zola wa kispaniola yupo
anaoza pale Old Trafford.
Mchezaji aliyekuwa na
uwezo wa kupiga pasi za mabao zenye wingi sawa na magoli ya Charlie
Austin leo hana uhakika wa maisha ya soka.
Mwandishi maarufu wa
Marekani mwanamama Erma Bombeck aliwahi kusema katika moja ya nukuu zake
kuwa Katika mwisho wa maisha yake atasimama mbele ya Mungu, na anaamini
hatokuwa na chembe yoyote ya kipaji chake ambayo hakuitumia na
angemwambia Baba nilitumia kila kitu ulichonipatia.
Alikuwa sahihi sana,
umaarufu na heshima aliyojiwekea vingekueleza hiki, hapa ndipo Mata
alipo, hili swali hata kwa Mungu litakuwa gumu Sana.
Kwa kipaji cha Mata
hajatumia walau nusu ya alichonacho. Bahati mbaya kwake sio yeye ambaye
anaamua kutokutumia kipaji, bali ana waamuzi kabla yake.
Tofauti na mwanamama
Bombeck ambaye maamuzi yalikuwa ndani ya kalamu na mkono wake Mata
maamuzi hayapo miguuni kwake, yapo akilini mwa makocha wake.
Uwezo wa kukaba wa
Valencia na young unaweka assist zake 15 kwa msimu benchi, Uwezo wa
Oscar na Willian kukimbia umbali mrefu uwanjani uliweka mchezaji bora
Mara mbili mfululizo wa klabu benchi.
Uliweka kipenzi cha
mashabiki na wapenzi wa soka benchi. Mchezaji aliyewanyima Usingizi
Carzola na Silva timu ya taifa akarudi benchi, akatulia.
Bahati mbaya Sana kwa
Mata, alikutana na wakufunzi viburi. Wasio sikia wala kuelewa. Dunia ya
Leo usipopendwa na Mourinho au Van Gaal ama wasipokusajili wao unahitaji
bahati ya Juu kuwa nacho wanachokitaka.
Wao ni wale Wanaoamini
kichwa Chao pekee. Mata hajawahi kuwa na nguvu ya Fellaini, hawezi
kukimbia mithili ya Hazard, na wala hawezi kaba kama Oscar lakini ana
Uwezo wa kupika mabao ambayo ndo kazi yake ya awali maradufu kuliko wote
hawa achilia mbali magoli anayoweza kukupa. Watu pekee ambao waliamini
miguu yake hawakupendwa ama kukubaliwa na wamiliki.
Di Matteo aliondoka,
Benitez hakuongezwa mkataba na tuliyemtegemea kukirudisha kiwango chake
David Moyes kibarua chake kilirithiwa mapema na Giggs kabla hajatulia
akatua mbabe ambaye anaweza kumweka Rooney beki na wala usimwambie kitu.
Ni dunia ya leo pekee
ambayo Liverpool hawamuhitaji Mata kwa sababu ya Sterling au Markovic,
na Manchester wanamlilia Fellaini dhidi ya Mata.
Ni kama ambavyo Kwenye maisha ya kawaida tunavyohitaji gari la kutembelea kuliko nyumba ya kuishi.
Mbabe wa zamani katika
siasa na uongozi katika nchi ya Ujerumani Adolf Hitler aliwahi kusema
Ufanye uongo uwe mkubwa, kisha Ufanye uwe mepesi, endelea kusema huo
uongo Mara nyingi na mwisho wa siku watu watauamini.
Ni kwa staili hii
ambayo alifanya watu waamini kuwa Ujerumani haikutakiwa kuchukuliwa kama
nchi zingine kwa mfano wa mama au mwanamke bali mwanaume,.
Uongo haswa lakini
uliokuja kuaminiwa na kutumika, aliwaua waisraeli na kufanya ukatili
ambao ulifanya kila nchi iamini Ujerumani in hatari achilia mbali
ukatili wa Marekani pale Japan ambao haujawahi kujirudia.
Hapa ndipo Mata alipo,
Mourinho alijaribu kusema, kisha akarudia, akafanya uwe rahisi na
mwisho tukaamini amini kuwa mata hakuwa mkabaji kama Oscar, ni kama
uongo wa Van Gaal ambao tumeuvumilia kisha kuukubali kuwa Young na
Valencia wanakupa kitu cha ziada ambacho Mata hakupi au Fellaini kimo
chake kinakupa mpango wa pili kufungua ulinzi wa upinzani.
Bahati mbaya Sana Kuna uongo ambao unaweza Kuja kuaminiwa kuwa Mata anatakiwa kwenda Juventus kwa sababu kakosa nafasi.
Mwisho atakosa jibu kwa
Mungu kuhusu kipaji chake maridhawa kama mwanamama Bombeck, atasema
nini wakati aliishia kufunga magoli 33 na kusaidia mengine 58 katika
mechi 135 Chelsea wakati alitakiwa awe na zaidi ya hapo.
Hata hivyo hakuna namna kama Hitler tu alivyosema, unadanganya, unasisitiza n unaufanya uongo uwe rahisi kisha unaaminiwa.
Hata kwa Mata tumeamua
kuamini, tunafurahia magoli ya Erikssen pale Tottenham, Coutinho pale
Liverpool na kusahau anayeyajua zaidi yupo benchi pale kwa mbabe Van
Gaal.
Ahsanteni.

