Mh.Zitto Kabwe alalamikia hatua za serikali zakutowatendea wakazi wa kilwa haki ili kunufaika na gesi.
Siku
moja baada ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anna
Makinda kusema kuwa Zitto Kabwe ni mbunge halali wa jimbo la Kigoma
Kaskazini kutokana na ofisi yake kutokuwa na taarifa rasmi ya
kutenguliwa ubunge wake, mbunge huyo leo amehudhuria mkutano wa bunge
unaoendelea mkoani Ddoma.
Katika siku hiyo ya kwanza ya kuhudhuria bungeni hapo mara baada ya
chama cha Demokrasia na Maendeleo -CHADEMA ambacho alikuwa mbunge
kupitia chama hicho kumfukuza uanachama Mhe.Zitto Kabwe amelalamikia
hatua ya Serikali kutowatendea haki wakazi wa Kilwa kwa kutowanufaisha
na gesi inayopatikana eneo hilo.