Meneja
wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Ofisi ya Mkoa wa
Lindi,Fortunata Raymond akitoa Mada ya Maboresho yanayotekelezwa na
Mfuko hususani kitita cha Mafao kwa Wanachama katika Kata namichiga
Wilayani Ruangwa ambapo pia aliwataka kutumia Mkutano huo kubainisha
Changamoto hasi na Chanya zitakazowezesha Maboresho Ya Huduma Za
Matibabu Sambamba Na Sekta Ya Afya Kwa Ujumla,Kushoto Katikati Ni
Mtendaji Kata Ya Namichiga Richard Nnonjela Na Kushoto Kabisa Ni Mwalimu
Mkuu Wa Shule Ya Msingi Namkonjera Iliyopo Kata Ya Namichiga.
Watumishi
Wa Kada Mbalimbali Ambao Ni Wanachama Wa Mfuko Wa Taifa Wa Bima Ya Afya
Waliopo Wilayani Ruangwa Katika Kata Ya Namichiga Wakimsikiliza Meneja
Wa Mfuko Wa Taifa Wa Bima Ya Afya Hayupo Pichani Wakati Wa Utekelezaji
Wa Mpango Wa Elimu Ya Kata Kwa Kata Sambamba Na Upimaji Wa Afya Kwenye
Magonjwa Yasiyoambukiza Ambapo Alisema Yamekuwa Ni Ya Gharama Kubwa Kwa
Kuwa Wengi Hawafahamu Dalili Zake Hivyo Uyafahamu Wakati Tayari
Yameshafikia Hatua Kubwa Ya Madhara Na Wakati Mwingie Kuchangia
Vifo,Hivyo Ofisi Ya Mkoa Wa Lindi Umekuwa Ukitekeleza Kwa Nia Ya
Kuongeza Uelewa Na Wanaobainika Kuwa Na Viashiria Kupata Ushauri Wa
Kitaalamu Kutoka Kwa Madaktari Wanaotoa Huduma.
Bi
Aisha Manjurungu Akipata Ushauri Wa Kitaalamu Kutoka Kwa Dk.Joyce Mmuni
Baada Ya Kupata Vipimo Ambapo Zoezi La Upimaji Afya Bure Kwa Wanachama
Wa Mfuko Na Wananchi Umetekelezwa Kwa Kutoa Huduma Ya Upimaji Kwenye
Magonjwa Yasiyoambukiza Kama Vile Kisukari,Presha Na Uwiano Wa Uzito Wa
Mwili Na Urefu,U Katika Viwanja Vya Gulioni Kata Ya Namichiga.
Wananchi
Wakipata Huduma Ya Upimaji Kwenye Banda La Mfuko Pichani Dkt.Grolia
Kiria Akimpima Bp Mmoja Kati Ya Mwananchi Aliyefika Kupata Huduma
Zilizokuwa Zikitolewa Mbali Na Upimaji Wananchi Walihamasishwa Kujiunga
Na Mfuko Wa Afya Ya Jamii (Chf).
Wananchi Waliojitokeza Kupata Huduma Wakiwa Kwenye Foleni.

