Ukizungumzia ujenzi wa nyumba za kuishi watu wengi wanaanza na kufikiria kuhusu mafundi, cement, mchanga na vifaa vingine… lakini upo ujenzi mwingine ambao mpaka unakamilika kabisa unaweza usihitaji chochote kati ya hivyo, labda akatakiwa fundi mmoja tu, naye ni wa kuchomelea !!
Joseph Dupuis
ni raia wa Canada ameunda nyumba yake ya kawaida kabisa kwa Kontena za
magari, kaokoa pesa nyingi sana kufanya makontena yake yawe nyumba ya
kuishi badala ya kujenga nyumba ya kawaida ya kuishi… jamaa anasema kitu
cha bei sana hapo ilikuwa hayo makontena pekeyake ambayo yaligharimu
kama Dola 12,600 (Sawa na kama Tshs. Mil. 26)
Ukiangalia kwa Dar, Tshs Milioni 26 ni pesa ambayo sio rahisi kupata nyumba ya kiwango kizuri.


0 comments:
Post a Comment