https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    ORODHA YA WACHEZA SOKA 10 WENYE MVUTO ZAIDI DUNIANI

    Ronaldo15Mtandao wa www.sokkaa.com umetoa orodha ya wanasoka 10 wenye mvuto aidi duniani ‘Most Handsome Footballers in the World’.
    Hii hapa ni orodha kamili;

    10. Mats Hummels-Borussi Drtmund 

    Der BVB im Trainingslager in Bad RagazMats Hummels ni mchezaji wa kijerumani anaekipiga kwenye klabu ya Dortimnd ambaye kwa sasa ni nahodha wa kikosi hicho. Ana mwonekano ambao wanawake wanaoshabikia mchezo wa mpira wa miguu wamekuwa wamekuwa na maswali mengi juu ya mwanandinga huyo.

    9. Gerrard Piqué–FC Barcelona 

    PiqueMacho yake ya blue na style ya nywele zake, Gerrard Pique anakamata nafasi ya tisa kwenye orodha ya  wachezaji wa mpira wenye mvuto zaidi.

    8. Cesc Fabregas-Chelsea 

    FabregasNi miongoni mwa viungo wachezeshaji kwenye ligi ya England (EPL) Mbali na uwezo wake wa kupiga pasi, Fabregas pia ni mwanaume mwenye mvuto na anashika namba nane kwenye orodha hii.

    7. Mario Gotze-Bayern Munich 

    GotzeNi kiungo wa klabu ya Bayern Munich ambaye alipata heshima kubwa nchini Ujerumani kwenye historia ya soka baada ya kufunga goli la ushindi kwa Ujerumani mwaka 2014 dhidi ya Argentina.

    6. Fernando Torres-Atletico Madrid 

    TorressFernando Tores a.k.a ‘El Nino’ amewatesa watoto wengi wa kike wanashabikia mpira kutokana na mvuto wa sura yake, stayle ya nywele na umbo la mwili wake ambalo limebalansiwa vizuri.

    5. Van Persie-Fenerbahce S.K. 

    van PersieRobin van Persie siku za hivi karibuni amepachikwa jina la utani ‘The Flying Dutchman’ kutokana na goli alilofunga kwa kichwa wakati Uholanzi inacheza dhidi ya Hispania kwenye michuano ya kombe la dunia mwaka 2014.

    4. Iker Casillas–Real Madrid  

    CasillasIker Casillas bado ni miongoni mwa magolikipa bora ulimwenguni na ni miongoni mwa wacheza mpira wenye mvuto zaidi duniani.

    3. David Villa–New York City FC

    VillaMbali na kufunga magoli mazuri, Villa amengia kwenye orodha ya wachezaji wenye mvuto pamoja na style nzuri ya nwele zake.

    2. Kaka–Orlando City FC

    KAKA1Ricardo Kaka anashika nafasi ya pili kwenye orodha hii. Muonekano wake wa kuvutia pamoja na style ya nywele, vilifungua milango ya yeye kuingia kwenye tasnia ya fashion. kampuni nyingi za fashion zimekuwa zikimsaka mkali huyo kwa ajili ya kufanya nae matangazo.

    1. Cristiano Ronaldo-Real Madrid

    RonaldoNyota huyo wa Real Madrid ni mchezaji wa mpira wa miguu mwenye mvuto zaidi duniani. Ni miongoni mwa wacheza mpira wachache ambao wanawafanya mashabiki wengi wa soka kuangalia mchezo huo. Mvuto wa sura, style ya nywele na umbo zuri ni baadhi ya vitu vinavyowachanganya watoto wa kike.
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ORODHA YA WACHEZA SOKA 10 WENYE MVUTO ZAIDI DUNIANI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top