Mshambuliaji
na mchezaji bora wa dunia Cristiano Ronaldo jana usiku alifunga magoli
mawili na kufikisha magoli 501 ya maisha yake ya soka huku pia akifikia
rekodi ya Raul Gonzalez ambaye alikua ndiye kinara wa mabao Madrid.
Ronaldo sasa amefikisha magoli
323 sawa na Raul Gonzalez aliyoifungia Real Madrid pekee na sasa
anatarajiwa kuweka rekodi yake binafsi ya ufungaji mara atakapofunga
tena katika mechi zijazo.
Ronaldo aliifungia Manchester
United magoli 118 huku akifungia Sporting Lisbon magoli 55. Ronaldo sasa
anakaribia kutengenezewa sanamu katika uwanja wa Santiago Bernabeu.


0 comments:
Post a Comment