https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    2015 Kumaliza Ubishi Kati Ya Pacquiao na Mayweather Junior


    Promota wa mchezo wa masumbwi Bob Arum, amethibitisha uwezekano wa magwiji wawili wa mchezo huo Manny Pacquiao pamoja na Floyd Mayweather Junior, kupanda ulingoni baadae mwaka
    huu.
    Arum, amethibitisha uwezekano huo baada ya kuweka hadharani taarifa za kukubali kwa Manny Pacquiao kupanda ulingoni kupitia kwa muwakilishi wake.
    Promota huyo amesema muwakilishi wa bondia huyo kutoka nchini Philippines amekubali dili ambalo litakamilisha mpango wake wa kutimiza lengo la kukabiliana na Mayweather ambae alikua akimuhutaji kwa miaka kadhaa iliyopita.
    Hata hivyo Bob Arum, amesema anaendelea na mazungumzo na upande wa Mayweather na anaamini atakubaliana na dili la kupanda ulingoni ambalo litaambatana na harakati za kusainiwa kwa mkataba wa pambano hilo.
    Mwishoni mwa juma lililopita taarifa kutoka katika vyombo mbali mbali vya habari vya mjini Las Vegas zilieleza kwamba kuna uwezekano mkubwa wa pambano la magwiji hao likafanyika katika ukumbi wa MGM Grand Garden May mbili mwaka huu.
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: 2015 Kumaliza Ubishi Kati Ya Pacquiao na Mayweather Junior Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top