Martin Odegaard akipozi katika picha na jezi yake wakati alipotambulishwa Real Madrid
NYOTA kinda wa Real Madrid mwenye umri wa miaka 16
aliyesajiliwa
kwa paundi milioni 2.3, Martin Odegaard amethitibisha kuwa hamu ya
kufanya kazi na Zinedine Zidane ndio imemfanya azipotezee timu za ligi
kuu England na kujiunga na mabingwa hao wa Ulaya.
Kinda
huyo wa Norwegian ambaye alitambulishwa katika uwanja wa klabu ya Real
Madrid, atakuwa anapokea mshahara wa paundi elfu 40,000 kwa wiki katika
msimu wake wa kwanza, lakini utaongezeka kutokana na Bonasi.
Amechagua
Real Madrid licha ya kuzitembelea klabu za Liverpool na Arsenal wakati
alipokuwa katika ziara ya kuziona timu kubwa barani ulaya.

