Wakala Jorge Mendes ameshindwa kukanusha uwezekano wa David de Gea kujiunga na Real Madrid
HATIMA
ya baadaye ya kipa wa Manchester United, David de Gea katika klabu hiyo
imekuwa kitendawili baada ya wakala wake kushindwa kukanusha tetesi za
kujiunga na Real Madrid majira ya kiangazi mwaka huu.
De
Gea amebakiza miezi 18 katika mkataba wake na bado hajaingia makubaliano
ya mkataba mpya ili aendelee kutumika Old Trafford na taarifa za kutua
Bernabeu zinazidi kuwa na uzito.
Wakala
wake, Jorge Mendes ambaye pia ni wakala wa Cristiano Ronaldo, aliulizwa
na vyombo vya habari vya Hispania kama kipa huyo mwenye miaka 24
anaweza kujiunga na Madrid.

