Alexis Sanchez akishangilia baada ya kuifungia Arsenal bao la pili dhidi ya Stoke City jumapili iliyopita
GWIJI
wa Arsenal, Thierry Henry amemtabiria mazuri Alexis Sanchez akitangaza
kuwa nyota huyo raia wa Chile atakuwa mrithi wa kufumania nyavu
Emirates.
Sanchez
ameanza kwa makali katika msimu wake wa kwanza wa ligi kuu England na
siku ya jumapili iliyopita Arsenal ikishinda 3-0 dhidi ya Stoke City
alikuwa moto wa kuotea mbali na alitia kambani gozi la ng’ombe.
Uwezo
wake wa kumalizia pasi za mwisho,kufunga na kasi yake ya umeme
kumesababisha watu wamfananishe na Henry, mshambuliaji mkubwa katika
historia ya klabu hiyo. Mfaransa huyo anaamini kumfananisha yeye na
Sanchez ni sahihi.

