https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    MUZIKI WA BONGO DANSI WAGEUKA MZIMU NA KUWAPELEKA PUTA WASHABIKI BARANI ULAYA

    ngoma
    Imebainika kuwa bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa band aka FFU-ughaibuni almaarufu viumbe wa ajabu Anunnaki Alien,inayoongoza na mwanamuziki Ebrahim Makunja aka kamanda Ras Makunja,bendi hiyo imejikuta ipo katika hali ya kukosa usingizi tena baada ya kutakiwa kutumbuiza maomyesho zaidi katika msimu ujao wa joto.

    Watayarishaji wa maonyesho makubwa ya nje barani Ulaya wanashinikizwa na washabiki wao lazima waipandishe jukwaani Ngoma Africa Band kutokana na mdundo wao Bongo dansi,maporota hao baada kuwekwa roho juu na washabiki wao nao wamedhamiria kuwapambanisha washabiki hao na bendi hiyo yenye makao yake nchini Ujerumani,habari za uhakika zimetonya kuwa bendi hiyo imekubali kuenda kutumbuiza katika nchi za Latvia na Austria na maonyesho mengine katika msimu wa joto.
    Habari zimetonya kuwa hali hiyo inatokana na tabia za washabiki kushinikiza bendi ya Ngoma Africa kuwepo katika ratiba ya mzunguko wa maonyesho makubwa pamoja na wanamuziki hao kukosa muda wa kupumzika.
    Hata hivyo inasemekana kamanda Ras Makunja na kikosi chake wanauwezo wa aina yake wa kuwamudu ratiba hiyo ngumu na kuwaburudisha washabiki wao waliodata akili na jinamizi la muziki wa dansi wa bongo kule barani ulaya.Ffu-Ughaibuni pia wanasikika online at www.ngoma-africa.com
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MUZIKI WA BONGO DANSI WAGEUKA MZIMU NA KUWAPELEKA PUTA WASHABIKI BARANI ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top