
Deontay Wilder sasa ndiyo gumzo kwa mabondia wanaoonekana kuwa tishio katika uzito wa juu katika ngumi za kulipwa.
Amefanikiwa kumchakaza mpinzani wake Bermane Stiverne kwa pointi katika mechi iliyopigwa kwenye jiji la Las Vegas, Marekani.
Katika
pambano hilo la ubingwa wa juu wa WBC, alishinda kwa pointi 118-109,
119-108 na 120-107, lakini kwa uwezo aliuonyesha. Basi wakali wengine
wakae chonjo.

