https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    TAFADHALI PICHA ZINATISHA:MAUAJI YA KUTISHA KITONGOJI CHA MKAGOBERO KIJIJI CHA KABANGA WILAYA YA NGARA MKOA WA KAGERA.

    Baadhi ya mashuhuda wakielekea eneo la tukio

    Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Shedrack Misago Ndironkeye(78) mkazi wa kitongoji cha Mkagobero kijiji cha kabanga wilayani Ngara mkoani kagera alikutwa ameuwawa kikatili  kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na baadhi ya sehemu za mwili wake kukatwa na kitu chenye ncha kali na watu wasiojulikana kisha  mwili wake kuutelekezwa kichakani huku kichwa kikiwa kimepondwa vibaya na kuwekewa kokoto.

    Mwili wa marehemu ukiwa umetelekezwa porini
    Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Alhamisi ya tarehe 26/03/2015, ambapo inadaiwa marehemu alikumbwa na mauti hayo akitokea kilabuni kuelekea nyumbani kwake majira ya usiku wa saa mbili nakuendelea. Kamanda wa polisi kituo cha Kabanga OCS Benard Joseph alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo jeshi la polisi linawasaka waliohusika na tukio hilo maana mpaka sasa hakuna mtu anayeshikiliwa kwa kuhusika na mauaji hayo.
    Mwili wa marehemu ukiwa umetelekezwa porini
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: TAFADHALI PICHA ZINATISHA:MAUAJI YA KUTISHA KITONGOJI CHA MKAGOBERO KIJIJI CHA KABANGA WILAYA YA NGARA MKOA WA KAGERA. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top