https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    ALAMA ZA WAABUDU SHETANI JE NDIO HIZII???????


    Mchungaji Joseph akiwa stendi ya Ubungo

    Kuna mtumishi kutoka Kenya yuko Dar es salaam anajulikana kama Mchungaji Joseph, amekuwa akizunguka vituo mbalimbali vya daladala akihubiri habari za Mungu na kusema mambo mbalimbali anayoyaita ni siri za shetani na kazi anazozifanya, Pia ni kwa jinsi gani watu wanachukuliwa misukule!
    Mtumishi huyu alielezea aina ya nguo ambazo zimetengenezwa kuzimu na Mtu akivaa hizi zenye wanyama hawa, huonekana moja kwa moja kwenye ramani ya kuzimu
    Alielezea kwamba aina ya nguo hizi mtu akivaa haishi miaka mingi, au kufa kifo kisicho cha kawaida
    Pia alielezea huyo mnyama yupo anaishi baharini hivyo hiyo siyo picha tu!
    Pia kulikua kuna kitambaa ambacho kilikua na alama mbalimbali ambazo anasema wanatumia wanaoabudu shetani au Freemasons. Na kusema pia wapo watu wanaosema ni wakristo wanatumia baadhi ya hizi alama hizi kwa kujua au kutokujua!
    Pia lisema kuna wahubiri wawili ambao wanahubiri kwenye TV wanahubiri na kuponya kwa nguvu za giza ambapo wanatumia PETE zenye nguvu za giza . Ameliasa kanisa kuombea kazi ya Mungu kwa kumaanisha maana wapo watu wamejiingiza kanisani kama kondoo kumbe ni mbwa mwitu.
    Alipokua akihitimisha mahubiri yake, alitaka watu watoe mafungu yao ya kumi na sadaka, pia aliwaombea wote waliokua na mahitaji mbalimbali.
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ALAMA ZA WAABUDU SHETANI JE NDIO HIZII??????? Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top