Twaha
Sultan akionyesha mpira anaotumia kwa ajili ya kujisaidia hali ambayo
inampa maumivu makali pamoja na kupata gharama kubwa ya kubadilisha
mpira kila baada ya wiki tatu.
Mama mdogo wa Sultan, Sarha akionyesha uvimbe unaomsumbua mtoto Twaha sultan.
Mwenyekiti
wa Taasisi ya Sitti Tanzania Foundation, Sitti Mtemvu akizungumza baada
ya kukabidhi msaada wa shs laki mbili kwa ajili ya kusaidia matibabu
yake.
Mwenyekiti
wa Taasisi ya Sitti Tanzania Foundation, Sitti Mtemvu (kushoto),
akimkabidhi msaada wa sh. laki mbili, Sarha Magamba, jijini Dar es
Salaam jana, kwa ajili ya kusaidia matibabu ya mtoto, Twaha Sultan (17),
mkazi wa Kipawa Karakata (katikati), ambaye ana uvimbe wa kilo nne na
nusu mgongoni.Yeyote atakayeguswa na tatizo la mtoto huyo anaweza
kuwasiliana na mlezi wake kupitia namba ya simu 0713970491.

