https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    Leo TANZANIA inaadhimisha Sherehe za Miaka 51 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar


    Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, leo anawaongoza watanzania katika kuadhimisha miaka 51 ya kuzaliwa kwa Tanzania baada ya kuunganisha nchi mbili huru za Tanganyika na Zanzibar.

    Katika‬ muungano huu ambao leo hii tunausherehekea nikwamba Mwalimu Nyerere alikuwa Rais wa kwanza na Kiongozi wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ),Sheikh Karume akawa makamu wa kwanza wa Rais.
     
    Baada ya tukio hilo sasa ambalo ni la kihistoria nchi ikaanza kutawaliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano ikitekeleza sheria zinazotolewa na Bunge la Tanzania.

    Nikukumbushe tu kwamba Mkataba wa muungano ulitiwa saini na aliyekuwa Rais wa Tanganyika Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere na aliyekuwa Rais wa Zanzibar Hayati Sheikh Karume Aprili 22,mwaka 1964 mjini Zanzibar.
     
    Bunge la Tanganyika na Baraza la Mapinduzi waliuthibitisha mkataba huo Aprili 26 na 27 mwaka 1964, viongozi wan chi hizo mbili walikutana katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam kubadilishana hati ya muungano.
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: Leo TANZANIA inaadhimisha Sherehe za Miaka 51 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top