https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    TIGO WAZINDUA HUDUMA MPYA YA INTERNET YA 4G LTE


    Wasanii wa vichekesho Bongo, Musa Kitale 'Mkude Simba' na Stan Bakola wakiingia katika ukumbi wa uzinduzi huo wa 4G LTE baada ya kupata maelekezo ya awali kutoka kwa
    wafanyakazi wa Tigo.
    Wasanii wa vichekesho Bongo, Musa Kitale 'Mkude Simba' na Stan Bakola wakiingia katika ukumbi wa uzinduzi huo wa 4G LTE baada ya kupata maelekezo ya awali kutoka kwa wafanyakazi wa Tigo.
    Wafanyakazi wa Kampuni ya Simu ya Huawei wakiuza simu zao katika uzinduzi huo wa Tigo wa netiweki ya 4G LTE.
    Ma MC wa sherehe ya uzinduzi huo wakitoa uafafanuzi katika hafla hiyo
    Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Tigo Tanzania, Cecile Tiano akizungumza jambo katika hafla hiyo.
    Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), John Nkoma akielezea namna ya uboreshwaji wa huduma za mawasiliano nchini unavyoendelea
    Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mbarawa (Mb) akizungumza jambo katika uzinduzi wa huduma hiyo mpya ya 4G LTEViongozi mbalimbali wakishudia jinsi netiweki ya 4G LTE inavyofanya kazi katika moja ya skrini
    Umati wa watu pamoja na wanahabari waliohudhuria hafla hiyo
    KAMPUNI ya mawasiliano ya Tigo imezindua huduma mpya ya kisasa ya ‘internet’ ya 4G LTE ambayo itakuwa ikipatikana nchini.

    Uzinduzi huo umefanyika leo katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mbarawa pamoja na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini, Prof. John Nkoma ambao waliungana kwa pamoja kwenye uzinduzi huo.

    Akizungumza katika uzinduzi huo wa internet ya 4G LTE, Mkuu wa Kitengo cha Internet wa Kampuni ya Tigo, David Zacharia alisema ‘netiweki’ hiyo ni ya kwanza kwa Tanzania na kwa mtumiaji wa mtandao huo anatakiwa kuwa na laini ya 4G na simu yenye uwezo wa kupokea 4G, tayari mteja huyo ataweza kupata huduma hiyo kwa kasi ya ajabu.

    Aidha, David alisema mteja ataweza kunufaika zaidi kutokana na uwezo wa kupokea data haraka, pia uwezo wake ni mara kumi (10) ya 3G (internet ya iliyozoeleka) na mteja atakaye kuwa tayari anaweza kujitapatia huduma zote kupitia vituo vyote vya Tigo kama Mlimani City, Masaki pamoja na maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar.
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: TIGO WAZINDUA HUDUMA MPYA YA INTERNET YA 4G LTE Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top