Timu ya soka ya FC Barcelona wamefanikwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu nchini Hispania hapo jana baada ya kuitungua Atletico Madrid kwa bao 1-0 katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa Vicente Calderon.
Bao pekee la Barcelona lilifungwa na mshambuliaji Lionel Messi katika dakika ya 65 ya mchezo huo.
Barcelona wametwaa ubingwa wakiwa na pointi 93 wakifuatiwa na Real Madrid wenye pointi 89 ili hali Atletico de Madrid wakiwa na pointi 77.







