.
Hata hivyo wakizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam
mmoja wa viongozi wa umoja huo, Bw James Mbatia wamewataka wananchi
wanaotaka madiliko kutokatishwa tamaa na changamoto hizo kwani
zinafanywa kwa lengo la kujaribu kudhoofisha vuguvugu la mabadiliko
jambo ambalo licha ya kuwa halitafanikiwa.
Aidha Mh Mbatia pia akalalamikia ukiukwaji wa taratibu za kufanya
kampeni ukiwemo wa kutumia lugha zinazochochea chuki na zinazoweza
kuligawa taifa.
Kwa nyakati tofauti, baadhi ya viongozi wa idara zinazolalamikiwa
akiwemo Bw, Paul Chagonja kutoka jeshi la polisi na jaji mkwawa kutoka
tume ya uchaguzi wameeleza baadhi ya malalamiko na pia wameendelea
kusisitiza suala zima la kila chama na kila mtanzania kuendelea
kuheshimu sheria na taratibu.
Kuhusu hofu iliyoanza kujengeka ya kutumia wizi wa kura unaodaiwa
kufanywa wakati wa uchaguzi Mh Jaji Mkuwawa amesema sheria ziko wazi na
zikifuatwa suala la kuibiwa kura halitakuwepo.
Akizungumza kwa njia ya simu kuhusu malalamiko ya UKAWA kuzuiliwa
kutumia uwanja wa Jangwani mkurugenzi wa manispaa ya Ilala amesema hana
taarifa rasmi za mabadiliko ya matumizi ya uwanja huo.


0 comments:
Post a Comment