https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    UNESCO, TCRA YATAKA WADAU WA HABARI KATIKA MATUMIZI YA INTANETI KUZINGATIA USIRI NA MAADILI

    IMG_8938
    Mwenyekiti wa National Governance Internet Forum ambaye pia ni Rais wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya akiwakaribisha wadau wa mitandao na watumiaji wa intaneti kwenye jukwaa hilo kabla ya kumkaribisha mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA kufungua rasmi jukwaa hilo.. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Tanzania Education and Research Network (TERNET), Amos Nungu na Kushoto ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph akifuatiwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bw. Sunday Richard. (Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
    IMG_9056
    Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bw. Sunday Richard akifungua rasmi Jukwaa la wadau wa usimamizi wa masuala ya mtandao (NIGF) lililoandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) na kufanyika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa mikutano COSTECH jijini Dar. Kushoto ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph aliyemwakilisha Mkurugenzi wa UNESCO na kulia Mwenyekiti wa National Governance Internet Forum, Kenneth Simbaya.
    IMG_8959
    Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph aliyemwakilisha Mkurugenzi wa UNESCO akitoa salamu za shirika la UNESCO wakati wa mkutano wa Jukwaa la wadau wa usimamizi wa masuala ya mtandao (NIGF) ulioandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC).

    IMG_9012
    Katibu Mtendaji wa Tanzania Education and Research Network (TERNET), Amos Nungu akitoa salamu za TERNET kwa wadau waliohudhuria jukwaa hilo.
    IMG_9203
    Mtaalamu kutoka TCRA Dk. Emmanuel Manasseh akiwasilisha mada iliyoelezea umuhimu wa mtandao katika maisha ya sasa na yajayo wakati wa jukwaa hilo.
    IMG_9206
    Pichani juu na chini ni sehemu ya washiriki waliohudhuria jukwaa hilo wakifuatilia "presentation" iliyokuwa ikitolewa na Mtaalamu kutoka TCRA Dk. Emmanuel Manasseh (hayupo pichani).
    IMG_9182
    IMG_9207
    IMG_8974
    IMG_9218
    Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph kwa mtaalamu kutoka TCRA (hayupo pichani) kama wana mipango gani kuhakikisha kuwa kutakuwepo na masafa ya kutosha kwa miaka mingi ijayo kwaajili ya wananchi wa vijijini na wale wasio na uwezo.
    IMG_9076
    Picha ya pamoja.
    IMG_9115
    Maxence Melo kutoka Jamii Forum akizungumza na waandishi wa habari wakati wa jukwaa lililowakutanisha kwa pamoja wadau wa masuala ya mitandao ya intaneti.
    IMG_9081
    Maxence Melo kutoka Jamii Forum (katikati) akipata picha ya pamoja na wajumbe wa Tanzania Bloggers Network (TBN), Fredy Njeje wa Blog za Mikoa (kulia) na Mr. Verbs.
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: UNESCO, TCRA YATAKA WADAU WA HABARI KATIKA MATUMIZI YA INTANETI KUZINGATIA USIRI NA MAADILI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top