Zaidi ya walimu 245,00 waliogoma
nchini Kenya watakosa mishahara yao ya mwezi Septemba baada ya
muajiri wao kutoa orodha ya malipo ya walimu 42,973 ambao ndio
watalipwa mishahara.
Tume ya Huduma za Walimu Kenya (TSC)
imechukua hatua hiyo wakati mahakama ya rufaa ya Kenya jana nayo
ikiwaagiza walimu kurejea shuleni na kuanza kufanyakazi mara moja.
Wengi wa walimu watakaolipwa
mishahara yao kamili ni wakuu wa shule, wasaidizi wao pamoja na wakuu
wa idara ambao walikuwepo shuleni wakati wote wa mgomo huo ulioanza
mwezi ulioisha.



0 comments:
Post a Comment