ARSENAL walifundishwa somo lingine usiku wa jana katika darasa la uwanja wa Nou Camp na FC Barcelona – waliongozwa na MSN.
Lionel
Messi, Luis Suarez na Neymar kama kawaida walikuwa kwenye orodha ya
wafungaji – kwa mara nyingine tena – wakati viongozi hao wa La Liga
wakifanikiwa kuvuka kwenda hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa wa
ulaya.
Wakatalunya waliitoa Gunners kwa ushindi wa jumla wa 5-1, wajumbe wa MSN pekee ndio waliofunga magoli hayo matano – Messi akifunga matatu, Neymar 1 na Suarez 1.
Kikosi
cha Arsene Wenger sio timu ya kwanza kukutana na kisago kilichosimamiwa
na MSN, na itakuwa sio timu ya kwanza kukumbana dhahama ya vijana hao
watatu wa KiAmerika ya kusini.
Mpaka kufikia sasa MSN wameshafunga magoli 106 msimu huu, yakiwemo magoli 68 katika La Liga pekee yake.
Idadi hii ni kubwa kuliko timu yoyote katika ligi kuu ya England katika msimu huu.
Timu zinazoongoza kwa kufunga magoli mengi katika Premier League msimu huu ni Leicester na Tottenham wakifunga magoli 53 — na kwa sasa ndio wanaongoza ligi kwa kushika nafasi ya kwanza na ya pili.
Messi, Suarez na Neymar wamefunga magoli 68 pekee yao kwenye La Liga msimu huu.
Lionel
Messi, Luis Suarez na Neymar kama kawaida walikuwa kwenye orodha ya
wafungaji – kwa mara nyingine tena – wakati viongozi hao wa La Liga
wakifanikiwa kuvuka kwenda hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa wa
ulaya.Wakatalunya waliitoa Gunners kwa ushindi wa jumla wa 5-1, wajumbe wa MSN pekee ndio waliofunga magoli hayo matano – Messi akifunga matatu, Neymar 1 na Suarez 1.
Kikosi
cha Arsene Wenger sio timu ya kwanza kukutana na kisago kilichosimamiwa
na MSN, na itakuwa sio timu ya kwanza kukumbana dhahama ya vijana hao
watatu wa KiAmerika ya kusini.
Mpaka kufikia sasa MSN wameshafunga magoli 106 msimu huu, yakiwemo magoli 68 katika La Liga pekee yake.Idadi hii ni kubwa kuliko timu yoyote katika ligi kuu ya England katika msimu huu.
Timu zinazoongoza kwa kufunga magoli mengi katika Premier League msimu huu ni Leicester na Tottenham wakifunga magoli 53 — na kwa sasa ndio wanaongoza ligi kwa kushika nafasi ya kwanza na ya pili.Messi, Suarez na Neymar wamefunga magoli 68 pekee yao kwenye La Liga msimu huu.


0 comments:
Post a Comment