June 04
2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli
amewaalika wawekezaji kutoka Jimbo la Jiangsu la nchini China kuungana
na Tanzania katika utekezaji wa mpango wa ujenzi wa viwanda na ujenzi wa
miundombinu hususani reli na amewahakikishia kuwa serikali yake ya
awamu ya tano itatoa ushirikiano wa karibu kufanikisha uwekezaji huo.
>>>.”Mheshimiwa
Luo Zhijun naomba uwaeleze wafanyabiashara wa Jimbo lako la Jiangsu
kwamba ninawakaribisha kwa mikono miwili, waje hata kesho waseme
wanataka kuanzisha kiwanda gani na sisi tutawapa ushirikiano”.
>>>”Tunayo
maeneo ya kutosha ya kuanzisha viwanda, kwa Pwani na Dar es salaam tuna
eneo la Bagamoyo tunaloweza kuweka viwanda zaidi ya 1,000 halikadharika
Kigamboni na maeneo mengine mengi katika mikoa mbalimbali nchini nzima” :- Rais Magufuli
Kwa upande
wake Luo Zhijun amemshukuru Rais Magufuli kwa utayari wake wa kuwapokea
wawekezaji kutoka Jimbo la Jiangsu na amemuahidi kuwa pamoja na kwamba
Jimbo hilo tayari limewekeza hapa nchini kiasi cha dola za Marekani
Bilioni 1 (Sawa na Shilingi Trilion 2.2) atahakikisha anawashawishi
wawekezaji wengi zaidi wa viwanda katika jimbo lake
Mazungumzo hayo yamehudhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda
ambaye June 03 2016 ametiliana saini makubaliano ya ushirikiano wa
kimaendeleo kati ya Mkoa wa Dar es salaam na Jimbo la Jiangsu ambapo
jimbo hilo limeahidi kuwekeza katika miradi mbalimbali ya viwanda vya
mazao ya kilimo, ujenzi na huduma za kijamii.


0 comments:
Post a Comment