Kiungo wa Chelsea ya Uingereza, Mhispaniola Cesc Fabregas ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kutengeneza mabao 15 katika misimu miwili huku akiikaribia rekodi ya kutengeneza mabao 20 yake mkongwe Thierry Henry
Fabregas alitengeneza nafasi ya 15 jumamosi katika pambano dhidi ya Swansea City ambapo walishinda 5-0 kunako dimba Liberty Stadium huku akikumbukwa kwa kutengeneza nafasi 17 alipokuwa na Arsenal msimu wa 2007-08 katika msimu mabo walimaliza nafasi ya tatu nyuma ya klabu yake ya sasa Chelsea na mabingwa wa msimu huo Manchester United
Kiujumla kitakwimu Fabregasi ametengeneza goli la 15 akiwa na Cheelsea toka alipohama Barcelona majira ya Kiangazi, amepangwa mara 21 sawa na dakika 1,851 minutes, amefunga goli 2, akijaribu lango mara 18, ametengeneza nafasi 67; amepiga jumla ya pasi 1,807 (ambapo usahihi ni sawa na 87%). Sasa amebakiza nafasi tano kumfikia Henry aliyemudu kufanya hivyo misimu 12 iliyopita.
.
na pengine nyota huyo angeweza kufikisha 16 kama siyo Diego Costa kuukosa mpira hatua chache toka lilipo lango la Swansea
Orodha kamili ya kutengeneza mabao ‘Assist’ kwa msimu mmoja ligi kuu ya Uingereza ni kama ifuatavyo
Idadi -Mchezaji (Msimu)
20 – Thierry Henry (2002-03)
18 – Frank Lampard (2004-05)
17 – Cesc Fabregas (2007-08)
16 – Eric Cantona (1992-93)
15 – David Silva (2011-12)
15 – Steve McManaman (1995-96)
15 – Matt Le Tissier (1994-95)
15 – Robert Pires (2001-02)
15 – David Beckham (1999-00)
15 – Cesc Fabregas (2014-15)
15 – Nobby Solano (1999-00)

