Gary
Neville amemshauri bosi wa Manchester United, Louis van Gaal kuendelea
kutumia mabeki wanne katika mechi zote zilizosalia msimu huu.
Mashetani
wekundu walianza na mabeki watatu wa kati katika ushindi wa 2-0 dhidi ya
QPR kwenye mechi ya jumamosi ya ligi kuu England, lakini walibadilisha
na kuingia katika mfumo wa mabeki wanne na hatimaye Marouane Fellaini na
James Wilson walifunga magoli kuipa pointi tatu Man United.
Mashabiki wa United hawapendi mfumo unaopendwa zaidi na Van Gaal wa 3-5-2 na Neville amewaunga mkono.

