https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    POLISI; WANANANCHI WANAFICHA WAHALIFU. WAGANGA WAKAMATWA NA NYARA ZA SERIKALI

    Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi.

     Baadhi ya ngozi za wanyama ambao ni nyara za serikali, zikiwa chini ya ulinzi mkali wa askari Polisi mkoani Mbeya, zinazosemekana zimekamatwa katika oparesheni ya kusaka waganga wa kienyeji wapiga ramli chonganishi.
     Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, akiwaonesha waandishi wa habari mkoani humo leo kucha za Chui na mbwa mdogo aliyekaushwa, vitu ambavyo amesema zimekamatwa kwa waganga wa kienyeji wapiga ramli chonganishi.

      Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi akionesha kucha za Chui.
      Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, akionesha baadhi ya vitu na tunguli zilizokamatwa kwa waganga wa jadi wapiga ramli chonganishi.


      Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, akionesha baadhi ya vitu na tunguli zilizokamatwa kwa waganga wa jadi wapiga ramli chonganishi.
    JESHI la Polisi mkoani Mbeya, limesema kuwa moja ya changamoto inayowakabili katika utendaji kazi zao, ni pamoja na baadhi ya wananchi kuwaficha wahalifu wakiwemo Waganga wa kienyeji wanaopiga ramli chonganishi.
    Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, ameyasema hayo leo ofisini kwake, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari na kutoa taarifa kuhusu msako unaoendelea wa kuwasaka na kuwakamata waganga wanaopiga ramli chonganishi mkoani hapa.

    Amesema katika oparesheni hiyo iliyoanza mwanzoni mwa mwezi huu, imefanikisha kukamatwa watuhumiwa 23 ambao baadhi yao wamefikishwa mahakamani na wengine wanaendelea kuhojia.

    Alivitaja baadhi ya vitu ambavyo wamekutwa navyo baadhi ya waganga hao kuwa ni pamoja na zana/vitendea kazi zikiwemo nyara za serikali.

    Baadhi ya nyara za serikali alizozitaja na kuzionesha mbele ya maafisa wa Jeshi hilo na baadhi ya waandishi wa habari kuwa ni Konokono 2 wa baharini, Mafuta ya Simba, Mifupa ya kakakuona, Vipande vitatu vya ngozi ya Chui, kucha za Chui, Mkia wa farasi, mifupa ya wanyama aina mbalimbali wa porini, kipande cha Nungunungu, mikia mitano ya paka pori na Pembe tatu za mnyama digidigi.

    Nyara zingine ni mguu mmoja wa Nyani, mguu mmoja wa ndege aina ya Tai, mguu mmoja wa mnyama aina ya Nyegere, Pembe nne za swala na Ngozi ya Mamba.

    Zana ambazo siyo nyara za serikali walivyokamatwa navyo alisema na kuvionesha kuwa ni Usinga, Biblia mbili za kabila la / Lugha ya Kinyasa, Mbwa mdogo aliyekaushwa kwa moshi, vitambaa. vioo, vibuyu vidogo vyenye shanga vikiwa na vitu vidhaniwavyo kuwa ni dawa asilia za aina mbalimbali, Fimbo nyeusi, msalaba na Pembe za Ng'ombe.

    Kamanda Msangi ametoa wito kwa jamii kujiepusha na tabia ya kusadiki imani potofu za kishirikina kwa kupiga ramli chonganishi kwa nia ya kutaka kutatua matatizo yao kwani hali hiyo inahatarisha usalama, umoja na mshikamano miongozi mwa jamii na kuleta chuki na uhasama, badala yake wamche Mungu.

    Aidha ameomba wananchi wenye taarifa za walipo waganga na wahalifu wengine kutoa taarifa kwa mamlaka husika ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: POLISI; WANANANCHI WANAFICHA WAHALIFU. WAGANGA WAKAMATWA NA NYARA ZA SERIKALI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top