https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    Rais Kikwete ateua wabunge wapya wawili

    TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewateua wabunge wawili (2) wapya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

    Walioteuliwa ni Dkt. Grace Khwaya Puja na Bwana Innocent Sebba.

    Rais amefanya uteuzi huu kwa mamlaka aliyopewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 66 (I) (e) ambapo amepewa mamlaka ya kuteua wabunge wasiozidi 10.

    Uteuzi huu umekamilisha idadi ya wabunge ambao Mheshimiwa Rais amepewa kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo Kikatiba.

    Wabunge ambao wameshateuliwa ni:


    • Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa
    • Mhe. Profesa Sospeter Mwijarubi Muhongo
    • Mhe. Dkt. Asha Rose Migiro
    • Mhe. Janet Zebedayo Mbene
    • Mhe. Saada Salum Mkuya
    • Mhe. Zakhia Hamdani Meghji
    • Mhe. Shamsi Vuai Nahodha
    • Mhe. James Fransis Mbatia


    Uteuzi huu umeanza tarehe 20 Machi, 2015.

    Imetolewa na:
    Premi Kibanga,
    Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi

    Ikulu-Dar-Es-Salaam
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: Rais Kikwete ateua wabunge wapya wawili Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top