Ndoa inasemekana ni baraka pale wachumba wanapokuwa wamependana kwa dhati,
na kwa hiari yao wanaona ni muda muafaka kuwa kitu kimoja kama mke na mume.
Lakini kwa upande mwingine ndoa inakuwa ni balaa na kupoteza maana pale wachumba wanapoamua kuingia katika ndoa bila sababu za msingi wala vigezo vya maana kati yao.
Yaani kila mmoja anaingia na sababu na mkakati wake tofauti na alionao mwenzake.