Tume
ya Taifa ya Uchaguzi imekanusha tuhuma kuwa baadhi ya wakurugenzi wa
NEC wameachishwa kazi ghafla na kazi zao wamepewa watu ambao
watakipendelea Chama cha Mapinduzi.
Mwenyekiti
wa Tume Jaji Lubuva amesema tuhuma zilizoibuliwa na Mwenyekiti wa
CHADEMA Freeman Mbowe hazina ukweli wowote na zinapotosha Umma.
Mbowe alisema kuwa maafisa wa Usalama wa Taifa wamepewa nafasi za uongozi ndani ya NEC
Jaji Lubuva amesema kuwa kuna
mabadiliko yalifanyika mwezi uliopita ambapo Rais Kikwete alimteua
Julius Malaba kuwa Mkurugenzi mpya wa Uchaguzi kwa lengo la kuimarisha
utendaji wa Tume na sio vinginevyo.
Jaji Lubuva ameomba baadhi ya viongozi wa kisiasa kuacha kuipotosha jamii


0 comments:
Post a Comment