Timu ya Manchester City imethibitisha kumnasa mshambuliaji wa Palmeiras, Gabriel Jesus kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 27.
Ikiwa ni baada ya saa 24 tangu kukamilisha uhamisho wa Leroy Sane kwa paundi milioni 37 kutoka Schalke, City wamewapiku Barcelona na kumnasa winga huyo Mbrazil Jesus, 19.
Kama ilivyo kuwa kwa Sane, Jesus ambaye analiwakilisha taifa lake katika michuano ya Olimpiki huko Rio amekubali mkataba wa miaka mitano, ila atabakia Palmeiras hadi Krismasi, wakati msimu wa soka wa Brazil utakapomalizika.




0 comments:
Post a Comment