Aaron Ramsey akishangilia na Alex Oxlade-Chamberlain, Olivier Giroud na Per Mertesacker kwenye uwanja wa Etihad
Jamie
Carragher amewaponda nyota wa Arsenal kwa kitendo cha kushangilia
kuzidi kiasi kufuatia kuifunga Manchester City jumapili iliyopita uwanja
wa Etihad.
Aaron
Ramsey ali-post picha katika mtandao wa Instagram akiwa yeye na
wachezaji wenzake Alex Oxlade-Chamberlain, Olivier Giroud na Per
Mertesacker wakiwa katika hali ya furaha kwenye vyumba vya kubadilishia
nguo.
Sio
huyo tu aliyekuwa ‘bize’ na mitandao ya kijamii kufuatia ushindi wa 2-0,
naye Alexis Sanchez alijipiga picha akiwa na marafiki zake.
Alexis Sanchez (juu) alijipiga picha akiwa na Mesut Ozil, Mathieu Flamini na Oxlade-Chamberlain
Hata
hivyo, kitendo hicho kimemfanya beki wa zamani wa Liverpool na
England, Jamie Carragher, aamini kuwa Arsenal wanatakiwa kuacha
kushangilia kupita kiasi mpaka watakaposhinda makombe kadhaa.
Carragher
ali-post picha yake akiwa na mchambuzi mwenzake wa Sky Sports , Gary
Neville baada ya kumaliza show, lakini aliwaambia Monday Night Football:
“Inanishangaza sana—huu ni utani mkubwa.
“Ilikuwa
mechi ya miamba miwili. Kiukweli unaweza kushangilia, lakini haina maana
kuweka mapicha mengi namna hii ya chumba cha kubadilishia nguo. Siku
zote picha zenye makombe ndio tamu, haina maana kwa mipicha hii na
wanatakiwa kuacha kufanya hivyo”.

