https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    Mkuu wa Wilaya Ilala Alilia Madawati.


    HALMASHAURI ya Manispaa ya Ilala imeendesha harambee ya uchangiaji wa madawati kwa shule zake za msingi 113.
     
    Akizungumza katika hafla ya uchangiaji wa madawati hayo iliyopewa jina la ‘Usiku wa Mswahili’ Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi alisema Halmashauri hiyo inakabiliwa na uhaba wa madawati yapatayo12,000.
     
    “Halmashauri yetu ina wanafunzi takriban 150,800 ambapo wanafunzi walioandikishwa darasa la kwanza kwa mwaka huu ni 22,000, baada ya kufanya tathmini tukagundua shule zetu zina uhaba wa madawati ndipo tukakubaliana kufanya harambee hii,” alisema.
     
    Alisema wadau mbalimbali wa elimu nchini wameitikia wito huo na kwamba tayari wamepata kupata kiasi cha madawati 1,173.
     
    “Hii inatia moyo kwamba tunaweza kumaliza changamoto hii tuliyonayo, hivyo nitoe wito kwa jamii kubadili mtazamo wao na kuanza kuchangia shughuli za kimaendeleo zenye tija kwa Taifa kama elimu na afya, hapa tunajenga rasilimali watu ambao watakuja kulitumikia Taifa  katika siku zijazo,” alisema.
     
    Kwa upande wake Ofisa Elimu Idara ya Elimu ya Msingi wilayani humo, Elizabeth Tomas alisema mbali na changamoto hiyo ya uhaba wa madawati pia wanakabiliwa na uhaba wa madarasa.
     
    “Tulitafakari… kwanini wanafunzi wanamaliza wakiwa na tatizo la mwandiko mbaya huku wengine wakiwa hawajui kusoma na kuandika tukagundua tatizo ni ukosefu wa madawati hasa kwa wale wanaoingia darasa la kwanza.
     
    “Hawa hulazimika kusomea yale ya wakubwa kwa maana hiyo tumejipanga kutengeneza ya kimo chao takriban madawati 5,231, tukimaliza hilo tutageukia upande wa madarasa,” alisema.
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: Mkuu wa Wilaya Ilala Alilia Madawati. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top