Na Simon Chimbo
Imeelezwa kuwa hali ya benchi la
ufundi la Chelsea sio nzuri kwa maana ya umoja na maelewano yaliyokuwepo
awali. Tangu Mourinho amfukuze katika benchi daktari mwanadada Eva
Carneiro hakuna maelewano mazuri miongoni mwa staffs.
Habari zinasema viongozi wote wa
klabu hawajapenda kitendo cha kocha Jose Mourinho kumnyanyasa Eva ambaye
alikua na mahusiano makubwa na viongozi pamoja na wachezaji.
Kutokana na kilichotokea, kocha
Jose Mourinho ambaye anashutumiwa kutumia maneno ya kibaguzi dhidi ya
mwanadada huyo, amekua kimya kuomba msamaha hadharani wala kujutia
maamuzi yake.
Mastaa wa Chelsea pia wengi
hawakupenda kilichotokea kwa daktari wao waliyemzoea na kuwa na
mahusiano ya karibu na kila mmoja wao kikosini.
Chelsea sasa imefungwa mechi tatu
huku ikitoa sare mechi moja na kushinda moja. Rekodi mbaya tangu mara
ya mwisho ilivyowatokea mwaka 1988.
Wiki hii bado ni ngumu na ya
mtego kwa Mourinho na Chelsea kwa ujumla. Wanacheza klabu bingwa
Jumatano hii dhidi ya Maccabi Tel Aviv ugenini kabla ya kuja kupambana
na Arsenal katika mchezo wa ligi kuu weekend ijayo.
Wachezaji wanaonekana kutokuwa na
njaa ya ushindi. Wamekata tamaa, wamechoka. Kuna maswali mengi nyuma ya
pazia kuona kama wachezaji hawa huenda wamechoka mbinu na tabia za
kocha wao. Ama kuna lolote kuhusiana na kutimuliwa kwa daktari wao?
Mechi dhidi ya Arsenal inaweza
kubadili kabisa upepo klabuni hapo. Chelsea na Mourinho wanahitaji
matokeo ili angalau kuleta furaha klabuni. Kama wakifungwa na Arsenal,
hakuna anayejua nini kipo kichwani mwa bosi Abramovich.
Wataalamu wa mambo ya kandanda
nchini England wanasema hakuna mchezaji hata mmoja anaecheza vizuri
kikosini hapo. Wachezaji wote wanaonekana hawana ari ya kujituma wala
ushindi.


0 comments:
Post a Comment