Viongozi wa Ulaya watajadili hatua
za kurahisisha mgogoro wa wahamiaji, huku Uturuki ikiwa ndio gumzo
katika jitihada hizo Jijini Brussels.
Karibu watu laki 6 wameingia nchi za
Umoja wa Ulaya kwa kutumia bahari hadi sasa katika kipindi cha mwaka
huu.
Uturuki inawahamiaji milioni 2,
wengi wao wakiwa wamekimbia vita katika nchi jirani za Syria.
Kuelekea mkutano huo Kansela wa
Ujerumani, Angela Merkel amehimiza umuhimu wa kuwepo kwa jitihada za
pamoja kukabiliana na mgogoro wa wahamiaji na kusema Uturuki
inajukumu muhimu.



0 comments:
Post a Comment