https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania


.

.

.
  • Latest News

    .

    Breaking News :Rais Magufuli Ateua Makatibu Tawala wa Mikoa 26


    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Aprili, 2016 amefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara.

    Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa kati ya Makatibu tawala hao 10 ni wapya, 2 wamebadilishiwa vituo vya kazi na 13 wamebakisha katika vituo vyao vya sasa.

    Makatibu Tawala wapya walioteuliwa ni kama ifuatavyo;

        1.Arusha -    Richard Kwitega
        2.Geita -      Selestine Muhochi Gesimba
        3.Kagera -     Armatus C. Msole
        4.Kilimanjaro -     Eng. Aisha Amour
        5.Pwani -      Zuberi Mhina Samataba
        6.Shinyanga -   Albert Gabriel Msovela
        7.Singida -     Dr. Angelina Mageni Lutambi
        8.Simiyu -    Jumanne Abdallah Sagini
        9.Tabora -   Dkt. Thea Medard Ntara
       10.Tanga -    Eng. Zena Said

    Makatibu Tawala waliobadilishwa vituo vya kazi ni kama ifuatavyo;

    1.Kigoma -   Charles Amos Pallangyo (Kutoka Mkoa wa Geita)
    2.Morogoro -  Dkt. John S. Ndunguru (Kutoka Mkoa wa Kigoma)

    Makatibu Tawala waliobakishwa katika vituo vyao vya sasa vya kazi ni kama ifuatavyo;

        1.Dar es salaam -  Theresia Louis Mbando
        2.Dodoma -     Rehema Hussein Madenge
        3. Iringa -   Wamoja Ayubu Dickolagwa
        4.Katavi -    CP Paul Chagonja
        5.Lindi -   Ramadhan Habibu Kaswa
        6.Mara -   Benedict Richard Ole Kuyan
        7.Manyara -     Eliakimu Chacha Maswi
        8.Mbeya-    Mariam Amri Mjunguja
        9.Mtwara -    Alfred Cosmas Luanda
       10.Mwanza -  CP. Clodwing Mathew Mtweve
       11.Njombe -   Jackson Lesika Saitabau
       12.Rukwa -   Symthies Emmanuel Pangisa
       13.Ruvuma -   Hassan Mpali Bendeyeko

    Makatibu Tawala wa Mikoa 10 ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza, wataapishwa siku ya Jumatano tarehe 27 Aprili, 2016 saa tatu asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam.

    Gerson Msigwa
    Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
    Dar es salaam
    25 Aprili, 2016
    https://play.google.com/store/apps/details?id=com.blog.ya.watanzania

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Breaking News :Rais Magufuli Ateua Makatibu Tawala wa Mikoa 26 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top